Swahili
Surah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Aya count 25
إِذَا السَّمَاءُ انشَقَّتْ
( 1 ) 
Itapo chanika mbingu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ
( 2 ) 
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ
( 3 ) 
Na ardhi itakapo tanuliwa,
وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ
( 4 ) 
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ
( 5 ) 
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ
( 6 ) 
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ
( 7 ) 
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا
( 8 ) 
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا
( 9 ) 
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ
( 10 ) 
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا
( 11 ) 
Basi huyo ataomba kuteketea.
وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا
( 12 ) 
Na ataingia Motoni.
إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا
( 13 ) 
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
إِنَّهُ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
( 14 ) 
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا
( 15 ) 
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ
( 16 ) 
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ
( 17 ) 
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ
( 18 ) 
Na kwa mwezi unapo pevuka,
لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍ
( 19 ) 
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
( 20 ) 
Basi wana nini hawaamini?
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩
( 21 ) 
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ
( 22 ) 
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ
( 23 ) 
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
( 24 ) 
Basi wabashirie adhabu chungu!
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ
( 25 ) 
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.