Swahili
Surah Al-Mursalat ( Those sent forth ) - Aya count 50
وَالْمُرْسَلَاتِ عُرْفًا
( 1 ) 
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
فَالْعَاصِفَاتِ عَصْفًا
( 2 ) 
Na zinazo vuma kwa kasi!
وَالنَّاشِرَاتِ نَشْرًا
( 3 ) 
Na zikaeneza maeneo yote!
فَالْفَارِقَاتِ فَرْقًا
( 4 ) 
Na zinazo farikisha zikatawanya!
فَالْمُلْقِيَاتِ ذِكْرًا
( 5 ) 
Na zinazo peleka mawaidha!
عُذْرًا أَوْ نُذْرًا
( 6 ) 
Kwa kuudhuru au kuonya,
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَاقِعٌ
( 7 ) 
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
فَإِذَا النُّجُومُ طُمِسَتْ
( 8 ) 
Wakati nyota zitakapo futwa,
وَإِذَا السَّمَاءُ فُرِجَتْ
( 9 ) 
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا الْجِبَالُ نُسِفَتْ
( 10 ) 
Na milima itakapo peperushwa,
وَإِذَا الرُّسُلُ أُقِّتَتْ
( 11 ) 
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
لِأَيِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ
( 12 ) 
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
لِيَوْمِ الْفَصْلِ
( 13 ) 
Kwa siku ya kupambanua!
وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الْفَصْلِ
( 14 ) 
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 15 ) 
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نُهْلِكِ الْأَوَّلِينَ
( 16 ) 
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ الْآخِرِينَ
( 17 ) 
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ
( 18 ) 
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 19 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ
( 20 ) 
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
فَجَعَلْنَاهُ فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ
( 21 ) 
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
إِلَىٰ قَدَرٍ مَّعْلُومٍ
( 22 ) 
Mpaka muda maalumu?
فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ الْقَادِرُونَ
( 23 ) 
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 24 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ كِفَاتًا
( 25 ) 
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
أَحْيَاءً وَأَمْوَاتًا
( 26 ) 
Walio hai na maiti?
وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ شَامِخَاتٍ وَأَسْقَيْنَاكُم مَّاءً فُرَاتًا
( 27 ) 
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 28 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
انطَلِقُوا إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ
( 29 ) 
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
انطَلِقُوا إِلَىٰ ظِلٍّ ذِي ثَلَاثِ شُعَبٍ
( 30 ) 
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
لَّا ظَلِيلٍ وَلَا يُغْنِي مِنَ اللَّهَبِ
( 31 ) 
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
إِنَّهَا تَرْمِي بِشَرَرٍ كَالْقَصْرِ
( 32 ) 
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
كَأَنَّهُ جِمَالَتٌ صُفْرٌ
( 33 ) 
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 34 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
هَٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ
( 35 ) 
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ
( 36 ) 
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 37 ) 
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَاكُمْ وَالْأَوَّلِينَ
( 38 ) 
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
فَإِن كَانَ لَكُمْ كَيْدٌ فَكِيدُونِ
( 39 ) 
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 40 ) 
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ
( 41 ) 
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ
( 42 ) 
Na matunda wanayo yapenda,
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
( 43 ) 
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
( 44 ) 
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 45 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
كُلُوا وَتَمَتَّعُوا قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجْرِمُونَ
( 46 ) 
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 47 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ارْكَعُوا لَا يَرْكَعُونَ
( 48 ) 
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 49 ) 
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
فَبِأَيِّ حَدِيثٍ بَعْدَهُ يُؤْمِنُونَ
( 50 ) 
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?