Swahili
Surah Al-Infitar ( The Cleaving ) - Aya count 19
إِذَا السَّمَاءُ انفَطَرَتْ
( 1 ) 
Mbingu itapo chanika,
وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انتَثَرَتْ
( 2 ) 
Na nyota zitapo tawanyika,
وَإِذَا الْبِحَارُ فُجِّرَتْ
( 3 ) 
Na bahari zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا الْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
( 4 ) 
Na makaburi yatapo fukuliwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
( 5 ) 
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ
( 6 ) 
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ
( 7 ) 
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
فِي أَيِّ صُورَةٍ مَّا شَاءَ رَكَّبَكَ
( 8 ) 
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِالدِّينِ
( 9 ) 
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَافِظِينَ
( 10 ) 
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
كِرَامًا كَاتِبِينَ
( 11 ) 
Waandishi wenye hishima,
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
( 12 ) 
Wanayajua mnayo yatenda.
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
( 13 ) 
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
وَإِنَّ الْفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٍ
( 14 ) 
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ الدِّينِ
( 15 ) 
Wataingia humo Siku ya Malipo.
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَائِبِينَ
( 16 ) 
Na hawatoacha kuwamo humo.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ
( 17 ) 
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ثُمَّ مَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ
( 18 ) 
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِّنَفْسٍ شَيْئًا ۖ وَالْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّهِ
( 19 ) 
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.